USHUHUDA WA ADELAIDA JUU YA MBINGU NA KUZIMU
Mwanamke mmoja kutoka Bolivia aitwaye Adelaida De Carrillo alipelekwa Mbinguni na Kuzimu na Yesu Kristo. Kule alionyeshwa ni Utakatifu gani anaotakiwa mtu kuwa nao ili aweze kuingia kwenye UFALME WA MUNGU, na pia ni dhambi gani (ambazo wengi wetu tunadhani kuwa ni ndogo), zinaweza kumfanya mtu aingie Jehanamu.
Tuko kwenye safari ya maisha ya kimwili h...apa duniani tukielekea kwenye maisha ya kiroho kwenye ulimwengu ule ujao. Huo ni ulimwengu halisi ambao una maisha halisi, utawala halisi na kanuni halisi za kuingia huko.
Wakati ulimwengu tuaoishi leo una serikali nyigi na watawala wengi, ulimwengu ule ujao utakuwa na serikali moja tu inayoongozwa na Yesu Kristo. Wakazi wa uliwengu huo ni watakatifu WOTE!!!
Huo ni ulimwengu unaoongozwa na Mungu mwenyewe kwa upendo na amani. Kule hakuna magonjwa, vita, njaa, na dhambi zingine zote. Tiketi ya kuingia kule ni moja tu: nayo ni kumwamini Yesu Kristo kama Mwokozi aliyekufa na kufufuka kwa ajili yetu. Kisha tunaishi hapa duniani kwa kutii maagizo yake.
Hata hivyo, wale wote ambao hawatakuwa wamestahili kuingia kwenye ulimwengu huo (kutokana na wao kuishi maisha ya dhambi na uasi dhidi ya sheria za Mungu hapa duniani), watatupwa nje ya mbingu kweny giza na moto, yaani kwenye jehanamu ya milele.
Katika ushuhuda huu, tunaona kile ambacho Bwana Yesu anatuagiza ili tuweze kustahili kuingia kwenye ufalme ule ujao na kuishi na Mungu MILELE!!!
Adelaida De Carrillo anasema:
HATUA YA 1: Ilianzia Kanisani kwenye wakati wa Huduma
Katika Ezekieli 36:25-26, Biblia inasema:
“Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote. Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.”
Ushuhuda wangu uko namna hii: Siku moja ya Jumapili, kwenye saa 3 hivi, Kanisa letu lilikuwa na kipindi cha Huduma. Mungu alikuwa akimimina baraka zake juu yetu. Mchungaji wangu aliniambia, “Adelaida, Bwana ananiambia nikupake mafuta.”
Aliweka mafuta mengi kwenye viganja vya mikono yake na akaanza kunipaka mwilini. Alinipaka masikioni, miguuni, tumboni na kwenye mwili wangu wote. Alipoweka mikono yake kwenye uso wangu, niliona mwanga mkubwa ukija kutokea juu, ukinielekea mimi. Kuanzia hapo nilipoteza fahamu na sikujua kilichokuwa kinaendelea kwangu.
HATUA YA 2: Safari Yangu Kwenda Mbinguni
Malaika walikuja na kunichukua tukaenda juu pamoja nao. Walianza kupambana na mashetani maana njia yetu ilikuwa imewekewa vizuizi. Kulikuwa na blangeti jeusi kwenye mawingu, likiwa limejaa mapepo yaliyojaribu kutuzuia kupita. Baadaye niliona mwanga mweupe kutoka Mbinguni na malaika mzuri sana akiwa na upanga wenye nuru mkononi mwake. Aliinua upanga wake na kuanza kupigana na mapepo yale ili sisi tupite. Malaika yule alionekana kama Mwana wa Mfalme. Alikuwa na bamba la dhahabu kifuani mwake na nguo nzuri sana. Nywele zake zilikuwa za rangi ya dhahabu, na uso wake ulikuwa kama miali ya mwanga. Alikuwa mzuri sana!
HATUA YA 3: Kuoshwa na Kubadilishwa Moyo Wangu
Malaika walikuja na kunichukua tukaenda juu pamoja nao. Walianza kupambana na mashetani maana njia yetu ilikuwa imewekewa vizuizi. Kulikuwa na blangeti jeusi kwenye mawingu, likiwa limejaa mapepo yaliyojaribu kutuzuia kupita. Baadaye niliona mwanga mweupe kutoka Mbinguni na malaika mzuri sana akiwa na upanga wenye nuru mkononi mwake. Aliinua upanga wake na kuanza kupigana na mapepo yale ili sisi tupite. Malaika yule alionekana kama Mwana wa Mfalme. Alikuwa na bamba la dhahabu kifuani mwake na nguo nzuri sana. Nywele zake zilikuwa za rangi ya dhahabu, na uso wake ulikuwa kama miali ya mwanga. Alikuwa mzuri sana!
Ghafla, nilisikia sauti ndani yangu, ikisema, “Nataka ufahamu kuwa nilikupa magoti hayo ili uwe mwanamke wa maombi, na si kwa ajili ya kuzungukazunguka ukifanya mambo yasiyonipendeza Mimi. Magoti haya ulipewa ili kufanya maombezi kwa ajili ya Kanisa. Ulitakiwa kulijua hilo.”
Kwa ujumla mimi nilikuwa si mwanamke wa maombi sana. Maombi yangu yalikuwa na kawaida ya kuwa mafupi sana. Lakini Bwana alitaka niwe mwombaji zaidi.
Malaika aliendelea kuosha miguu yangu, huku akiiparua, na mimi nilikuwa namlilia Mungu anihurumie kutokana na maumivu yale. Bwana akasema: “Miguu hii ulipewa ili uwe unazunguka kwenda kuhubiri Injili yangu, kueneza Neno langu na si kuzungukazunguka kwa majirani zako kupeleka umbeya, na kufanya mambo ambayo hayanipendezi Mimi. Na kwa sababu hii,” Bwana akasema, “ninasafisha miguu yako.”
Jambo hili liliendelea na lilifanyika kwa maumivu makali sana. Bwana akasema, “Hii ni muhimu sana ili uweze kuelewa mipango niliyo nayo kwa ajili yako.”
Baadaye, nilipelekwa kwenye sehemu nyingine ambako malaika wngine watatu walikuwa wananingojea. Sehemu hii ilikuwa tofauti. Niliona vitu kama mashine. Malaika wale walianza mchakato mwingine wa kusafisha macho yangu kwa kutumia aina fulani ya mafuta. Nilihisi kama vile macho yameng’olewa kutoka kwenye matundu yake. Nikasema: “Tafadhali mnihurumie. Naomba msaada. Kwa nini mnanifanyia hivi?” Ilikuwa kama vile wanakwangua macho yangu. Kitu kama samaki kilitolewa kutoka kwenye macho yangu.
Bwana akasema, “Binti yangu, nafanya hivi kwa ajili yako kwa sababu nataka ubadilike. Mambo uliyokuwa ukifanya duniani hayakuwa yakinipendeza. Sikuwa nafurahi ukiwa duniani ulipokuwa ukitazama mambo ambayo hayakunipendeza Mimi. Ulikuwa ukitazama TV” [Soap Operas] ... “Hayo hayajengi maisha yako.” ... “Sifurahii pale wanangu wanapoangalia vitu kama hivyo; vitu ambavyo havinipi utukufu.”
Nikasema, “Bwana, nisamehe. Naomba rehema zako.” Na Bwana akasema, “Katikati ya usiku kwenye saa sita, mara zote huwa uko macho ukiangalia sinema ambazo hazikujengi wewe; na nyingi ya sinema hizo zimejazwa mambo mengi yanayohusu mapenzi. Sikukupa macho hayo kwa ajili ya mambo kama hayo. Nilikupa hayo macho ili utazame mambo yale tu yanayonipa Mimi utukufu. Na kwa sababu hii ndiyo maana ninasafisha macho yako.”
Malaika waliendelea kusafisha macho yangu huku mimi nikiendelea kuomba kuhurumiwa. Baadaye macho yangu yalipakwa mafuta, na kuanzia hapo nikawa na mtazamo tofauti; macho yangu yalibadilishwa kabisa. Bwana akasema, “Usitamani waume wa watu wengine tena!” Mimi nilikuwa na kawaida ya kuvutiwa sana na wanaume wengine, na Bwana alisema kuwa mambo hayo hayampendezi.
Nitakueleza mimi nilikuwa mtu wa namna gani. Nilikuwa Mkristo duni wa kilokole ambaye alikuwa hatendi mambo sawasawa na Biblia inavyoagiza. Kila nilichofanya kilikuwa ni kutokana na matamanio yangu na njia zangu binafsi, kinyume kabisa na mapenzi ya Mungu. Nakueleza haya ili uweze kurekebisha njia zako; ili roho ziweze kuokolewa. Nakueleza kuwa tamaa NI dhambi; kuangalia michezo ya kwenye TV [Soap Operas], sinema za kidunia – mambo yote haya hayampendezi Mungu.
Malaika waliendelea na mchakato wa usafishaji. Walikuwa na kijifimbo kidogo cha kioo ambacho walikiingiza moja kwa moja masikioni mwangu. Walipoanza kukwangua masikio yangu, nilihisi maumivu makali sana. Moyo wangu ulihisi maumivu haya yote. Mara maji meusi yalianza kutoka kwenye masikio yangu, na baadaye maji ya rangi ya kijivu. Niliendelea kulia.
Bwana akasema, “Binti yangu, ninasafisha masikio yako kwa sababu ulipenda sana kusikiliza mambo ambayo hayanipendezi Mimi. Ulipenda kusikiliza umbeya. Uliyatoa kabisa masikio yako kusikiliza mambo yasiyonipendeza Mimi. Baadhi ya watu wanakuja kwako kuleta umbeya na wewe ulipenda kuwasikiliza hata kama walileta umbeya dhidi ya Mchungaji wako mwenyewe. Ulipenda kuwasikiliza hao. Badala ya kumtetea Mchungaji wako na kumsahihisha mbeya huyo ili arekebishe njia zake, ulikuwa kama wao, ukifanya umbeya pamoja nao. Usisikilize umbeya tena. Mtu akija kwako na umbeya wa aina yoyote, waombe radhi, kisha ondoka mara moja bila kushiriki. Usisikilize tena mambo yasiyokujenga!”
Nikasema: “Bwana, nisamehe!” Nilijua kuwa nilikuwa nina hatia. Hakuna jambo lililofichika mbele za Mungu. Hakuna anayeweza kujificha mbele zake. Kila tunachofanya na kusema hapa duniani kimewekwa kumbukumbu Mbinguni. Kutokana na maumivu yote yale masikioni mwangu, nikasema: “Bwana, nisamehe. Naomba rehema zako.” Hatimaye masikio yangu yalipakwa mafuta na malaika.
Bwana akaniambia: “Kuanzia leo na kuendelea, utasikiliza tu mambo ambayo nimekuruhusu kusikiliza. Utafanya mambo yale tu ambayo nimekutaka ufanye; hautakuwa Adelaida wa zamani tena. Hivi sasa wewe ni mtu mpya na ni lazima uwe ni mwanamke yule ambaye ninataka uwe.”
Baada ya hapo nilipelekwa kwenye idara nyingine ambako malaika walianza kusafisha kinywa changu. Ulimi wangu ulitolewa kabisa kinywani na kuwekwa kwenye aina fulani ya sinia. Malaika alianza kusafisha ulimi wangu, na hapa tena nilihisi maumivu makali sana. Bwana akasema: “Nataka kukusafisha. Nataka kukusafisha.”
Malaika walivyokuwa wanakwangua ulimi wangu, maji meusi yalikuwa yanatoka humo, na baadaye yalitoka maji meupe. Mwishowe malaika walitumia maji matamu sana kuoshea ulimi wangu. Yalikuwa matamu mno. Hakuna kitu duniani kinachoweza kulinganishwa na utamu wa maji yale. Kisha ulimi wangu ulipakwa mafuta. Kinywa changu nacho kilipitia mchakato huohuo. Maji meusi yalitoka kwenye kinywa changu.
Bwana akasema, “Binti yangu, ninafanya hivi kwa ajili yako ili usifanye umbeya tena; ili uache kufanya mambo yasiyonipendeza; maana ulimi wako ulishiriki katika mambo mengi sana ambayo hayanipi utukufu Mimi. Ulisema uongo mwingi sana. Acha kusema uongo! Kusema uongo hakutoki kwangu. Waongo hawanipendezi Mimi. Waongo wote hawataniona Mimi. Hakuna mwongo atakayeingia kwenye Ufalme wa Mbinguni.”
Nikasema: “Bwana, nihurumie. Najua kuwa nilifanya mambo hayo yote. Nilisema uongo mara nyingi, lakini tafadhali nisamehe.” Nilisema yote haya kwa sababu ya maumivu niliyokuwa nayahisi.
Bwana akasema: “Ninafanya hivi kwa sababu ninakupenda. Ukiendelea na hali uliyokuwa nayo, nitakupoteza. Kama nisingefanya yote haya, usingebadilika kamwe. Ni lazima niokoe moyo wako na hii ndiyo sababu ya kufanya yote haya. Nakupenda, na kwa sababu nakupenda, sitaki kukupoteza.”
Bwana akasema tena: “Kama ulivyo wewe, wengi kati ya watu wangu wako namna hiyohiyo.Wanasema uongo, wanaishi maisha ya aina mbilimbili, na wanaonekana wako safi mbele ya watu wengine. Unapomwinulia mumeo sauti ulimi wako unakuwa unatumiwa pia.” Kinywa changu kilitakaswa kabisa. Halafu Bwana akaniambia nimeze maji hayo. Nami nikafanya hivyo.
Ulimi wangu na kinywa changu vilipakwa mafuta ya thamani sana ya mbinguni. Mafuta hayo yalikuwa maalum sana, yakiwa na harufu ya thamani sana. Hayawezi kulinganishwa na mafuta yoyote ya hapa duniani. Ulimi wangu ulirudishwa tena kinywani mwangu. Malaika mmoja alikuja na kuweka hatamu kwenye koo langu. Na Bwana akaniambia: “Hii ni sawa na vile farasi anavyowekewa hatamu.”
Nikwambie tu kwamba, hii ndiyo njia pekee tunayoweza kubadilishwa. Acha kuongea maneno machafu na kushiriki katika mambo ambayo hayatujengi. Mambo haya hayampendezi Mungu kamwe.
Acha kutamka maneno machafu na yasiyo na maana. Wako Wakristo wengi – akina kaka, dada, Wainjilisti, Wamisionari, n.k., ambao wanapenda kusema maneno machafu na yasiyo na maana. Niko hapa kukuhakikishia juu ya kile ambacho Bwana alinionyesha ili maisha yako yabadilishwe. Ushuhuda huu ni kwa ajili ya wewe kubadilika. Upendo wa Mungu na wa kwangu kwako ndio ulioleta ushuhuda huu.
Ulimi wangu ulirudishiwa tena mahali pake na malaika na ukawa umebadilishwa kabisa. Naweza kukuambia sasa, hakuna mtu anayeweza kunikasirisha tena. Sasa naweza kufanya yale tu yanayompendeza Mungu.
Kisha, pua yangu nayo ilipitia mchakato huohuo. Maji meusi yalitoka puani mwangu wakati wa kusafishwa na baadaye maji meupe. Pua yangu ilipakwa mafuta na nilihisi maumivu makali sana wakati wa mchakato wa kusafishwa. Nilisema: “Bwana, tafadhali niambie mambo niliyofanya kwa kutumia pua yangu ambayo hayakukupendeza.”
Bwana akaniambia: “Baadhi ya wateja wako huvuta sigara na wewe unavuta ule moshi kupitia pua zako maana uliwahi kuwa mvutaji sigara na sasa wewe unajisikia vizuri kukaa nao wakati wanapovuta.” Nikasema: “Bwana, najua. Nisamehe. Naomba unirehemu.”
Bwana akaniambia: “Uko sawa tu na wale wote wanaovuta sigara na wote wanaokunywa pombe pale unapokaa nao na kuvuta harufu ya sigara na pombe.”
Bwana akasema tena: “Hii ndiyo sababu yangu ya kukusafisha wewe. Kwa hiyo, kuanzia leo kila utakapomwona mtu anavuta sigara au anakunywa pombe, hautajisikia vizuri kukaa nao tena. Utajisikia kinyaa.”
Hakuna cha kujitetea mbele za Bwana. Mungu anafahamu fika wewe ni nani na mimi ni nani. Libarikiwe Jina Takatifu la Bwana, Amina.
Niliendelea kumwomba Bwana rehema na nilipelekwa sehemu nyingine. Pale, malaika walianza kuosha mwili wangu uliobakia kwa kutumia sabuni nyeupe. Maji ya kijivu yalitoka kwenye mwili wangu.
Nikasema: “Bwana, nisaidie. Tafadhali, nisaidie.” Malaika walikuwa wanasugua mwili wangu na ngozi ya juu iliondoka. Damu ilikuwa inachuruzika kutoka kwenye ngozi yangu na nikamwuliza Bwana: “Kwa nini unanifanyia hivi?”
Bwana akaniambia: “Ninakusafisha. Ni lazima uwe safi mwili wako wote, nafsi yako, na roho yako. Roho yako, nafsi na mwili ni lazima viwe safi, asema Bwana.”
Sabuni ilisuuzwa kutoka kwenye ngozi yangu kwa kutumia maji ya thamani sana. Kisha malaika walipaka mafuta kila sehemu ya mwili wangu; kila sehemu ya mwili wangu. Sehemu zote za mwili wangu zilipakwa mafuta.
Bwana akaniambia: “Usirudi tena kwenye njia zako za zamani, binti yangu. Hivi sasa wewe ni Mtakatifu wangu aliyepakwa mafuta.”
Nikasema: “Bwana, nisamehe kwa mambo yote niliyokuwa nikifanya zamani hata mbele za uwepo wako. Nisamehe Bwana kwa kuwa kila kitu ambacho Mchungaji wangu alijaribu kunisahihisha mimi nilikuwa nikipingana naye. Nilisema mambo mengi kwake ambayo sikutakiwa kusema.”
Mchungaji wangu mara nyingi alikuwa akiniambia kuwa mavazi yangu kama Mkristo hayakuwa sawa. Nilishindana naye sana. Aliwahi kuniambia kuwa nilisema uongo na mimi nikahuzunika. Pale mtu anapopotoka na Mchungaji wake akamsahihisha, mtu huyo huhuzunika. Siku zote mimi nilikuwa kinyume na Mchungaji wangu.
Kisha nilipelekwa kwenye idara nyingine ambako nilipokelewa na malaika watatu. Malaika wale walitumia nguo nyeupe kufuta maji kwenye mwili wangu. Kwenye nyuso za malaika wale, niliona kuwa walikuwa wanajisikia huruma sana kwa ajili yangu kutokana na yote niliyopitia lakini hawakusema kitu chochote, hata neno moja. Sikuweza kumwona Bwana kwenye sehemu hizi. Nilikuwa nasikia tu sauti yake.
Malaika wengine watatu walinipokea kwenye idara nyingine. Malaika hawa walinivika nguo nyeupe ya juu na sketi ndefu. Sketi ilikuwa ndefu sana kiasi kwamba miguu yangu ilikuwa haionekani.
Je, Baada ya Kuvishwa nguo hizo alikwenda wapi, na pengine alikuwa na nani?
*****inaendelea sehemu ya Pili*****
Mwanamke mmoja kutoka Bolivia aitwaye Adelaida De Carrillo alipelekwa Mbinguni na Kuzimu na Yesu Kristo. Kule alionyeshwa ni Utakatifu gani anaotakiwa mtu kuwa nao ili aweze kuingia kwenye UFALME WA MUNGU, na pia ni dhambi gani (ambazo wengi wetu tunadhani kuwa ni ndogo), zinaweza kumfanya mtu aingie Jehanamu.
Tuko kwenye safari ya maisha ya kimwili h...apa duniani tukielekea kwenye maisha ya kiroho kwenye ulimwengu ule ujao. Huo ni ulimwengu halisi ambao una maisha halisi, utawala halisi na kanuni halisi za kuingia huko.
Wakati ulimwengu tuaoishi leo una serikali nyigi na watawala wengi, ulimwengu ule ujao utakuwa na serikali moja tu inayoongozwa na Yesu Kristo. Wakazi wa uliwengu huo ni watakatifu WOTE!!!
Huo ni ulimwengu unaoongozwa na Mungu mwenyewe kwa upendo na amani. Kule hakuna magonjwa, vita, njaa, na dhambi zingine zote. Tiketi ya kuingia kule ni moja tu: nayo ni kumwamini Yesu Kristo kama Mwokozi aliyekufa na kufufuka kwa ajili yetu. Kisha tunaishi hapa duniani kwa kutii maagizo yake.
Hata hivyo, wale wote ambao hawatakuwa wamestahili kuingia kwenye ulimwengu huo (kutokana na wao kuishi maisha ya dhambi na uasi dhidi ya sheria za Mungu hapa duniani), watatupwa nje ya mbingu kweny giza na moto, yaani kwenye jehanamu ya milele.
Katika ushuhuda huu, tunaona kile ambacho Bwana Yesu anatuagiza ili tuweze kustahili kuingia kwenye ufalme ule ujao na kuishi na Mungu MILELE!!!
Adelaida De Carrillo anasema:
HATUA YA 1: Ilianzia Kanisani kwenye wakati wa Huduma
Katika Ezekieli 36:25-26, Biblia inasema:
“Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote. Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.”
Ushuhuda wangu uko namna hii: Siku moja ya Jumapili, kwenye saa 3 hivi, Kanisa letu lilikuwa na kipindi cha Huduma. Mungu alikuwa akimimina baraka zake juu yetu. Mchungaji wangu aliniambia, “Adelaida, Bwana ananiambia nikupake mafuta.”
Aliweka mafuta mengi kwenye viganja vya mikono yake na akaanza kunipaka mwilini. Alinipaka masikioni, miguuni, tumboni na kwenye mwili wangu wote. Alipoweka mikono yake kwenye uso wangu, niliona mwanga mkubwa ukija kutokea juu, ukinielekea mimi. Kuanzia hapo nilipoteza fahamu na sikujua kilichokuwa kinaendelea kwangu.
HATUA YA 2: Safari Yangu Kwenda Mbinguni
Malaika walikuja na kunichukua tukaenda juu pamoja nao. Walianza kupambana na mashetani maana njia yetu ilikuwa imewekewa vizuizi. Kulikuwa na blangeti jeusi kwenye mawingu, likiwa limejaa mapepo yaliyojaribu kutuzuia kupita. Baadaye niliona mwanga mweupe kutoka Mbinguni na malaika mzuri sana akiwa na upanga wenye nuru mkononi mwake. Aliinua upanga wake na kuanza kupigana na mapepo yale ili sisi tupite. Malaika yule alionekana kama Mwana wa Mfalme. Alikuwa na bamba la dhahabu kifuani mwake na nguo nzuri sana. Nywele zake zilikuwa za rangi ya dhahabu, na uso wake ulikuwa kama miali ya mwanga. Alikuwa mzuri sana!
HATUA YA 3: Kuoshwa na Kubadilishwa Moyo Wangu
Malaika walikuja na kunichukua tukaenda juu pamoja nao. Walianza kupambana na mashetani maana njia yetu ilikuwa imewekewa vizuizi. Kulikuwa na blangeti jeusi kwenye mawingu, likiwa limejaa mapepo yaliyojaribu kutuzuia kupita. Baadaye niliona mwanga mweupe kutoka Mbinguni na malaika mzuri sana akiwa na upanga wenye nuru mkononi mwake. Aliinua upanga wake na kuanza kupigana na mapepo yale ili sisi tupite. Malaika yule alionekana kama Mwana wa Mfalme. Alikuwa na bamba la dhahabu kifuani mwake na nguo nzuri sana. Nywele zake zilikuwa za rangi ya dhahabu, na uso wake ulikuwa kama miali ya mwanga. Alikuwa mzuri sana!
Ghafla, nilisikia sauti ndani yangu, ikisema, “Nataka ufahamu kuwa nilikupa magoti hayo ili uwe mwanamke wa maombi, na si kwa ajili ya kuzungukazunguka ukifanya mambo yasiyonipendeza Mimi. Magoti haya ulipewa ili kufanya maombezi kwa ajili ya Kanisa. Ulitakiwa kulijua hilo.”
Kwa ujumla mimi nilikuwa si mwanamke wa maombi sana. Maombi yangu yalikuwa na kawaida ya kuwa mafupi sana. Lakini Bwana alitaka niwe mwombaji zaidi.
Malaika aliendelea kuosha miguu yangu, huku akiiparua, na mimi nilikuwa namlilia Mungu anihurumie kutokana na maumivu yale. Bwana akasema: “Miguu hii ulipewa ili uwe unazunguka kwenda kuhubiri Injili yangu, kueneza Neno langu na si kuzungukazunguka kwa majirani zako kupeleka umbeya, na kufanya mambo ambayo hayanipendezi Mimi. Na kwa sababu hii,” Bwana akasema, “ninasafisha miguu yako.”
Jambo hili liliendelea na lilifanyika kwa maumivu makali sana. Bwana akasema, “Hii ni muhimu sana ili uweze kuelewa mipango niliyo nayo kwa ajili yako.”
Baadaye, nilipelekwa kwenye sehemu nyingine ambako malaika wngine watatu walikuwa wananingojea. Sehemu hii ilikuwa tofauti. Niliona vitu kama mashine. Malaika wale walianza mchakato mwingine wa kusafisha macho yangu kwa kutumia aina fulani ya mafuta. Nilihisi kama vile macho yameng’olewa kutoka kwenye matundu yake. Nikasema: “Tafadhali mnihurumie. Naomba msaada. Kwa nini mnanifanyia hivi?” Ilikuwa kama vile wanakwangua macho yangu. Kitu kama samaki kilitolewa kutoka kwenye macho yangu.
Bwana akasema, “Binti yangu, nafanya hivi kwa ajili yako kwa sababu nataka ubadilike. Mambo uliyokuwa ukifanya duniani hayakuwa yakinipendeza. Sikuwa nafurahi ukiwa duniani ulipokuwa ukitazama mambo ambayo hayakunipendeza Mimi. Ulikuwa ukitazama TV” [Soap Operas] ... “Hayo hayajengi maisha yako.” ... “Sifurahii pale wanangu wanapoangalia vitu kama hivyo; vitu ambavyo havinipi utukufu.”
Nikasema, “Bwana, nisamehe. Naomba rehema zako.” Na Bwana akasema, “Katikati ya usiku kwenye saa sita, mara zote huwa uko macho ukiangalia sinema ambazo hazikujengi wewe; na nyingi ya sinema hizo zimejazwa mambo mengi yanayohusu mapenzi. Sikukupa macho hayo kwa ajili ya mambo kama hayo. Nilikupa hayo macho ili utazame mambo yale tu yanayonipa Mimi utukufu. Na kwa sababu hii ndiyo maana ninasafisha macho yako.”
Malaika waliendelea kusafisha macho yangu huku mimi nikiendelea kuomba kuhurumiwa. Baadaye macho yangu yalipakwa mafuta, na kuanzia hapo nikawa na mtazamo tofauti; macho yangu yalibadilishwa kabisa. Bwana akasema, “Usitamani waume wa watu wengine tena!” Mimi nilikuwa na kawaida ya kuvutiwa sana na wanaume wengine, na Bwana alisema kuwa mambo hayo hayampendezi.
Nitakueleza mimi nilikuwa mtu wa namna gani. Nilikuwa Mkristo duni wa kilokole ambaye alikuwa hatendi mambo sawasawa na Biblia inavyoagiza. Kila nilichofanya kilikuwa ni kutokana na matamanio yangu na njia zangu binafsi, kinyume kabisa na mapenzi ya Mungu. Nakueleza haya ili uweze kurekebisha njia zako; ili roho ziweze kuokolewa. Nakueleza kuwa tamaa NI dhambi; kuangalia michezo ya kwenye TV [Soap Operas], sinema za kidunia – mambo yote haya hayampendezi Mungu.
Malaika waliendelea na mchakato wa usafishaji. Walikuwa na kijifimbo kidogo cha kioo ambacho walikiingiza moja kwa moja masikioni mwangu. Walipoanza kukwangua masikio yangu, nilihisi maumivu makali sana. Moyo wangu ulihisi maumivu haya yote. Mara maji meusi yalianza kutoka kwenye masikio yangu, na baadaye maji ya rangi ya kijivu. Niliendelea kulia.
Bwana akasema, “Binti yangu, ninasafisha masikio yako kwa sababu ulipenda sana kusikiliza mambo ambayo hayanipendezi Mimi. Ulipenda kusikiliza umbeya. Uliyatoa kabisa masikio yako kusikiliza mambo yasiyonipendeza Mimi. Baadhi ya watu wanakuja kwako kuleta umbeya na wewe ulipenda kuwasikiliza hata kama walileta umbeya dhidi ya Mchungaji wako mwenyewe. Ulipenda kuwasikiliza hao. Badala ya kumtetea Mchungaji wako na kumsahihisha mbeya huyo ili arekebishe njia zake, ulikuwa kama wao, ukifanya umbeya pamoja nao. Usisikilize umbeya tena. Mtu akija kwako na umbeya wa aina yoyote, waombe radhi, kisha ondoka mara moja bila kushiriki. Usisikilize tena mambo yasiyokujenga!”
Nikasema: “Bwana, nisamehe!” Nilijua kuwa nilikuwa nina hatia. Hakuna jambo lililofichika mbele za Mungu. Hakuna anayeweza kujificha mbele zake. Kila tunachofanya na kusema hapa duniani kimewekwa kumbukumbu Mbinguni. Kutokana na maumivu yote yale masikioni mwangu, nikasema: “Bwana, nisamehe. Naomba rehema zako.” Hatimaye masikio yangu yalipakwa mafuta na malaika.
Bwana akaniambia: “Kuanzia leo na kuendelea, utasikiliza tu mambo ambayo nimekuruhusu kusikiliza. Utafanya mambo yale tu ambayo nimekutaka ufanye; hautakuwa Adelaida wa zamani tena. Hivi sasa wewe ni mtu mpya na ni lazima uwe ni mwanamke yule ambaye ninataka uwe.”
Baada ya hapo nilipelekwa kwenye idara nyingine ambako malaika walianza kusafisha kinywa changu. Ulimi wangu ulitolewa kabisa kinywani na kuwekwa kwenye aina fulani ya sinia. Malaika alianza kusafisha ulimi wangu, na hapa tena nilihisi maumivu makali sana. Bwana akasema: “Nataka kukusafisha. Nataka kukusafisha.”
Malaika walivyokuwa wanakwangua ulimi wangu, maji meusi yalikuwa yanatoka humo, na baadaye yalitoka maji meupe. Mwishowe malaika walitumia maji matamu sana kuoshea ulimi wangu. Yalikuwa matamu mno. Hakuna kitu duniani kinachoweza kulinganishwa na utamu wa maji yale. Kisha ulimi wangu ulipakwa mafuta. Kinywa changu nacho kilipitia mchakato huohuo. Maji meusi yalitoka kwenye kinywa changu.
Bwana akasema, “Binti yangu, ninafanya hivi kwa ajili yako ili usifanye umbeya tena; ili uache kufanya mambo yasiyonipendeza; maana ulimi wako ulishiriki katika mambo mengi sana ambayo hayanipi utukufu Mimi. Ulisema uongo mwingi sana. Acha kusema uongo! Kusema uongo hakutoki kwangu. Waongo hawanipendezi Mimi. Waongo wote hawataniona Mimi. Hakuna mwongo atakayeingia kwenye Ufalme wa Mbinguni.”
Nikasema: “Bwana, nihurumie. Najua kuwa nilifanya mambo hayo yote. Nilisema uongo mara nyingi, lakini tafadhali nisamehe.” Nilisema yote haya kwa sababu ya maumivu niliyokuwa nayahisi.
Bwana akasema: “Ninafanya hivi kwa sababu ninakupenda. Ukiendelea na hali uliyokuwa nayo, nitakupoteza. Kama nisingefanya yote haya, usingebadilika kamwe. Ni lazima niokoe moyo wako na hii ndiyo sababu ya kufanya yote haya. Nakupenda, na kwa sababu nakupenda, sitaki kukupoteza.”
Bwana akasema tena: “Kama ulivyo wewe, wengi kati ya watu wangu wako namna hiyohiyo.Wanasema uongo, wanaishi maisha ya aina mbilimbili, na wanaonekana wako safi mbele ya watu wengine. Unapomwinulia mumeo sauti ulimi wako unakuwa unatumiwa pia.” Kinywa changu kilitakaswa kabisa. Halafu Bwana akaniambia nimeze maji hayo. Nami nikafanya hivyo.
Ulimi wangu na kinywa changu vilipakwa mafuta ya thamani sana ya mbinguni. Mafuta hayo yalikuwa maalum sana, yakiwa na harufu ya thamani sana. Hayawezi kulinganishwa na mafuta yoyote ya hapa duniani. Ulimi wangu ulirudishwa tena kinywani mwangu. Malaika mmoja alikuja na kuweka hatamu kwenye koo langu. Na Bwana akaniambia: “Hii ni sawa na vile farasi anavyowekewa hatamu.”
Nikwambie tu kwamba, hii ndiyo njia pekee tunayoweza kubadilishwa. Acha kuongea maneno machafu na kushiriki katika mambo ambayo hayatujengi. Mambo haya hayampendezi Mungu kamwe.
Acha kutamka maneno machafu na yasiyo na maana. Wako Wakristo wengi – akina kaka, dada, Wainjilisti, Wamisionari, n.k., ambao wanapenda kusema maneno machafu na yasiyo na maana. Niko hapa kukuhakikishia juu ya kile ambacho Bwana alinionyesha ili maisha yako yabadilishwe. Ushuhuda huu ni kwa ajili ya wewe kubadilika. Upendo wa Mungu na wa kwangu kwako ndio ulioleta ushuhuda huu.
Ulimi wangu ulirudishiwa tena mahali pake na malaika na ukawa umebadilishwa kabisa. Naweza kukuambia sasa, hakuna mtu anayeweza kunikasirisha tena. Sasa naweza kufanya yale tu yanayompendeza Mungu.
Kisha, pua yangu nayo ilipitia mchakato huohuo. Maji meusi yalitoka puani mwangu wakati wa kusafishwa na baadaye maji meupe. Pua yangu ilipakwa mafuta na nilihisi maumivu makali sana wakati wa mchakato wa kusafishwa. Nilisema: “Bwana, tafadhali niambie mambo niliyofanya kwa kutumia pua yangu ambayo hayakukupendeza.”
Bwana akaniambia: “Baadhi ya wateja wako huvuta sigara na wewe unavuta ule moshi kupitia pua zako maana uliwahi kuwa mvutaji sigara na sasa wewe unajisikia vizuri kukaa nao wakati wanapovuta.” Nikasema: “Bwana, najua. Nisamehe. Naomba unirehemu.”
Bwana akaniambia: “Uko sawa tu na wale wote wanaovuta sigara na wote wanaokunywa pombe pale unapokaa nao na kuvuta harufu ya sigara na pombe.”
Bwana akasema tena: “Hii ndiyo sababu yangu ya kukusafisha wewe. Kwa hiyo, kuanzia leo kila utakapomwona mtu anavuta sigara au anakunywa pombe, hautajisikia vizuri kukaa nao tena. Utajisikia kinyaa.”
Hakuna cha kujitetea mbele za Bwana. Mungu anafahamu fika wewe ni nani na mimi ni nani. Libarikiwe Jina Takatifu la Bwana, Amina.
Niliendelea kumwomba Bwana rehema na nilipelekwa sehemu nyingine. Pale, malaika walianza kuosha mwili wangu uliobakia kwa kutumia sabuni nyeupe. Maji ya kijivu yalitoka kwenye mwili wangu.
Nikasema: “Bwana, nisaidie. Tafadhali, nisaidie.” Malaika walikuwa wanasugua mwili wangu na ngozi ya juu iliondoka. Damu ilikuwa inachuruzika kutoka kwenye ngozi yangu na nikamwuliza Bwana: “Kwa nini unanifanyia hivi?”
Bwana akaniambia: “Ninakusafisha. Ni lazima uwe safi mwili wako wote, nafsi yako, na roho yako. Roho yako, nafsi na mwili ni lazima viwe safi, asema Bwana.”
Sabuni ilisuuzwa kutoka kwenye ngozi yangu kwa kutumia maji ya thamani sana. Kisha malaika walipaka mafuta kila sehemu ya mwili wangu; kila sehemu ya mwili wangu. Sehemu zote za mwili wangu zilipakwa mafuta.
Bwana akaniambia: “Usirudi tena kwenye njia zako za zamani, binti yangu. Hivi sasa wewe ni Mtakatifu wangu aliyepakwa mafuta.”
Nikasema: “Bwana, nisamehe kwa mambo yote niliyokuwa nikifanya zamani hata mbele za uwepo wako. Nisamehe Bwana kwa kuwa kila kitu ambacho Mchungaji wangu alijaribu kunisahihisha mimi nilikuwa nikipingana naye. Nilisema mambo mengi kwake ambayo sikutakiwa kusema.”
Mchungaji wangu mara nyingi alikuwa akiniambia kuwa mavazi yangu kama Mkristo hayakuwa sawa. Nilishindana naye sana. Aliwahi kuniambia kuwa nilisema uongo na mimi nikahuzunika. Pale mtu anapopotoka na Mchungaji wake akamsahihisha, mtu huyo huhuzunika. Siku zote mimi nilikuwa kinyume na Mchungaji wangu.
Kisha nilipelekwa kwenye idara nyingine ambako nilipokelewa na malaika watatu. Malaika wale walitumia nguo nyeupe kufuta maji kwenye mwili wangu. Kwenye nyuso za malaika wale, niliona kuwa walikuwa wanajisikia huruma sana kwa ajili yangu kutokana na yote niliyopitia lakini hawakusema kitu chochote, hata neno moja. Sikuweza kumwona Bwana kwenye sehemu hizi. Nilikuwa nasikia tu sauti yake.
Malaika wengine watatu walinipokea kwenye idara nyingine. Malaika hawa walinivika nguo nyeupe ya juu na sketi ndefu. Sketi ilikuwa ndefu sana kiasi kwamba miguu yangu ilikuwa haionekani.
Je, Baada ya Kuvishwa nguo hizo alikwenda wapi, na pengine alikuwa na nani?
*****inaendelea sehemu ya Pili*****
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni